WAPO LYRICS BY NAY WA MITEGO


Free Nation It’s a Nine Double Six baby huh

Unacho kipanda leo ndicho utachovuna kesho
Imeandikwa mwanaume kula kwa jasho
Najiuliza hivi nani kaiona kesho
Chapa mwendo na ukilala hauna chako
Hivi uhuru wa kuongea kwenye nchi bado upo
Nsije kuongea vitu kesho nikajikuta Central…

Kuna viongozi wavuta bangi wapo maana wana maamuzi ya kifee wapo
Walio mmiss Jakaya wapo na waliochoka kuisoma namba wapo
Kuna wasanii mateja wapo na waliopoteza marinda wapo ah

Kuna radio na tv naona vimeshapoteza CV uh
Hakuna uhuru wa habari wala taarifa ya habari
Wanapindisha pindisha kuiogopa serikali hah
Siamini nchi inaendeshwa kwa kiki
Siasa inafunika muziki viongozi wanashindana kukiki
Wanagombea front page wauze kwenye gazeti

Nasikia kuna viongozi wame forge vieti wapo kuna mademu wanasagana wapo
Eti kuna vidume vinalelewa wapo sijasikia mnasema wapo
Kuna ma staa wanajiuza wapo wapenda habari za udaku kuliko kazi wapo
Eti kuna wasanii wanarogana wapo sijasikia mnasema

Kiongozi mwenye busara anapokea ushauri
Anapokea mawazo haweki mbele kiburi
Haya samahani muheshimiwa hivi unamjua Bashite
Hili ni jipu jipya toka Koromije
Limeshaiva na usaa limeshatunga nakukabidhi sindano ya kulidunga
Daktari haogopi kubwa kidonda we si doctor wa majipu
Tumbua hakuna kuvunga
Kuvamia ofisi za watu hee kumbe nayo ni kazi
Hakuna noma wanangu tupige kazi bodaboda kazi Bajazi kazi
Eti vipi kukaba nayo ni kazi

Nasikia kuna viongozi wame forge vieti wapo kuna mademu wanasagana wapo
Eti kuna vidume vinalelewa wapo sijasikia mnasema wapo
Refa ni wao piga manati chapaa vita ya masai na mang’ati fire
Biashara ya ngono na super shafti ahaa pumzi imekata nashika shati (sudibidii)
Siamini nchi inaendeshwa kwa kiki
Siasa inafunika muziki viongozi wanashindana kukiki
Wanagombea front page wauze kwenye gazeti

Kuna viongozi wavuta bangi wapo maana wana maamuzi ya kifee wapo
Walio mmiss Jakaya wapo na waliochoka kuisoma namba wapo
Nasikia kuna viongozi wame forge vieti wapo kuna mademu wanasagana wapo
Eti kuna vidume vinalelewa wapo sijasikia mnasema wapo

Hahaa aah we mtu gani sasa? Hutaki kushauriwa hutaki kukosolewa
Umerogwa wewe! Unajiona ndugu yake na Yesu eeh eeh!
Oya wanangu eeh round hii mtanyooka haki ya Mungu
Naona kichaa kapewa rungu

Ayaa also mkifanyiwa piga manati vita ya masai na mang’ati
Pesa na ngono na super shafti pumzi imekata nashita shati
Chapaa…. Fire… Utakula jeuri yako ahaa! Free Nation

Mi ndo yule afcast wa kinyakyusa na kichaga
Oya Amosi Seja! Mbeya City one love hahaa The True Boy Is In The Building

No comments:

Post a Comment