KWETU LYRICS BY RAYVANNY

 
                

Sifa kwa Mola wangu Maulana kwa mengi aliofanya 
Hadi mi na we kukutana, kisura

Sijapanga kudanganya, ntasema ukweli mama
Kisa nakupenda sana, kisura
Umesema wanipenda ila maisha yangu maseke
Michicha, milenda ndo menyu yangu, na ya kuku mateke
Yaani chenga, kila siku kilio sa lini nicheke?
Sina tenda, ugali Buguruni, mboga Temeke
Nafurahi umeniridhia niwe na wewe kimwali
Maisha yangu mitihani isoisha maswali
Ukifika nyumbani vumilia maana hali sio swali
Asubuhi mchana pakavu, jioni ndo kula futali

[Pre-Chorus]
Tena huku kwetu muda wowote mateja wanatinga
Viwalo vyetu ukifua kumbuka kuvilinda
Huku kwetu muda wowote mateja wanatinga
Mwali wee, suala la nyumba na gari mimi

[Chorus]
Bado, mi bado, mi bado
Ndo kwanza nimepanga
Bado, iyee, mi bado
Sina hata kiwanja
Bado, iyee, mi bado
Kulipa kodi majanga
Bado, mimi bado, mi bado

[Verse 2]
Mtaani kwetu hekaheka ukienda sokoni kariri vichochoro
Ghetto na mkeka tu hakuna kitanda, shuka wala godoro
Hekaheka hakuna kibatari ndani giza totoro
Mvua ikinyesha nyumba inageuka ka boti ya Comoro
Ila nimeshakupa, nimeshakupa mtima mtima
Ukija kususa, utanizika mzima mzima
Nimeshakupa eh, nimeshakupa mtima mtima
Ukija kususa ah, utanizika mzima mzima

[Pre-Chorus]
Tena huku kwetu muda wowote mateja wanatinga
Viwalo vyetu ukifua kumbuka kuvilinda
Huku kwetu muda wowote mateja wanatinga
Mwali wee, suala la nyumba na gari mimi

[Chorus]
Bado, mi bado, mi bado
Ndo kwanza nimepanga
Bado, iyee, mi bado
Sina hata kiwanja
Bado, mie, mi bado
Kulipa kodi majanga
Bado, mimi bado, mi bado
Suala la nyumba na gari mimi

Bado, mi bado, mi bado
(Haki ya Mungu bado, yaani shuka bado)
Ndo kwanza nimepanga
Bado, iyee, mi bado
Sina hata kiwanja
Bado, iyee, mi bado
Kulipa kodi majanga
Bado, mimi bado, mi bado

No comments:

Post a Comment